Thursday, 10 August 2017

ODINGA AISHANGAZA TUME KWA KUJITANGAZIA MATOKEO.

Tume ya Uchaguzi ya Kenya imesema ni mapema na ni kinyume cha sheria kwa mgombea wa upinzani Raila Odinga kujitangazia kuwa ameshinda uchaguzi wa Kenya.
Alhamisi, muungano wa upinzani wa NASA ulichapisha matokeo ambayo yanaonyesha kuwa Raila Odinga amemshinda Rais wa sasa Uhuru Kenyatta, ambapo pia waliitaka tume ya uchaguzi imtangaze Odinga kuwa ndiye Rais mteule.
Hata hivyo matokeo ya awali hadi sasa yaliyotangazwa na tume hiyo yanaonyesha Rais wa sasa Uhuru Kenyatta bado anaongoza dhidi ya mpinzani wake Raila Odinga.
Source:bbcswahili
Na:Esko Donald.

No comments:

Post a Comment

JIFUNZE KUPITIA HADITHI.

…JESCA…… Episode 4 Na:Esko Donald Esko Wa Simulizi 'EWS' Whatsapp:0675730796 Ilipoishia… Kwa muda huo watu wote walikuwa wapo ...