Watu 25 wamefariki dunia na wengine takriban 20 wamejeruhiwa kutokana na moto mkubwa uliozuka katika msitu uliopo katikati mwa nchi ya Ureno.
Kwa mujibu wa taarifa ya awali iliyotolewa na serikali ya nchi hiyo imedai, watu wengi walifariki wakati walipokuwa wakijaribu kuyakimbia maeneo ya Pedrogao Grande yaliyopo Kusini Mashariki mwa mji wa Coimbra.
Naye waziri wa mambo ya ndani wa nchi hiyo, João Gomes amewaambia waandishi habari kuwa watu 16 wameteketea ndani ya magari yao hadi kufa, pale walipokabiliwa na moto huo mkubwa katika Wilaya ya Pedrógão Grande katika barabara inayounganisha miji ya Figueiro dos Vinhos na Castanheira de Pera.
Wakati huo huo waziri mkuu António Luís Santos da Costa, amesema hilo ni tukio baya zaidi kuwahi kutokea nchini humo katika miaka ya hivi karibuni.
Source:Bongo5
Na:Esko Donald.
Sunday, 18 June 2017
25 WAFARIKI KWA MOTO URENO.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
JIFUNZE KUPITIA HADITHI.
…JESCA…… Episode 4 Na:Esko Donald Esko Wa Simulizi 'EWS' Whatsapp:0675730796 Ilipoishia… Kwa muda huo watu wote walikuwa wapo ...

-
Linapojatwa jina la Director Nisher bila shaka itakuwa unakumbuka video ya nyimbo ya Young D "Kijukuu" na nyingine nyingi ambazo z...
-
Madrid yafanikiwa kuandika historia mpya baada ya kulichukua kombe hili mara mbili mfululizo.
-
Na:Esko Donald. Esko Wa Simulizi 'EWS'. Jesca binti wa Kimasai mwenye rangi ya bahati kuliko mabinti wote kijijini kwao alikuwa ni...
-
Bila shaka ni wengi hatumfahamu Lemma Guya Gemeda,huyu ni mchoraji maarafu kutoka nchini Ethiopia.Lemma ana umri wa miaka 90 na amechora zai...
-
……JESCA…… Episode ya 2 Na:Esko Donald. Esko Wa Simulizi 'EWS'. Whatsapp:0675730796. Ilipoishia.. BAADA YA MIAKA MITATU. Jesca...
No comments:
Post a Comment