Saturday, 6 May 2017

POLISI ARUSHA WATHIBITISHA NI ZAIDI YA WATU 30 WALIOFARIKI KWENYE AJALI LEO.

Kamanda wa Polisi mkoani Arusha Charles Mkumbo amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema idadi ya waliofariki ni 32 akiwemo dereva kwenye kundi la watu wazima watatu,wavulana ni 12 na wasichana ni 17.Ajali hii imetokea Leo May 6,2017 kwenye eneo la Mlima Rhotia,Karatu mkoani Arusha.
Imeripotiwa kuwa ajali hii ilihusisha basi la wanafunzi ambao walikuwa wanakwenda kufanya mtihani wa ujirani mwema.
Inasemekana dereva wa basi hilo aliyejulikana kwa jina la Luck Vicent alishindwa kuliongoza vizuri basi hilo wakati akikata kona kwenye mteremko hivyo lilimshinda na kuingia kwenye korongo na kusababisha umauti wa roho 32.
Na:Esko Donald.

No comments:

Post a Comment

JIFUNZE KUPITIA HADITHI.

…JESCA…… Episode 4 Na:Esko Donald Esko Wa Simulizi 'EWS' Whatsapp:0675730796 Ilipoishia… Kwa muda huo watu wote walikuwa wapo ...