Monday, 9 October 2017

JIFUNZE KUPITIA HADITHI.

…JESCA……
Episode 4
Na:Esko Donald
Esko Wa Simulizi 'EWS'
Whatsapp:0675730796

Ilipoishia…
Kwa muda huo watu wote walikuwa wapo kwenye usingizi mzito unaweza kusema hawataamka tena,kila mmoja alikuwa anakoroma mithili ya mlevi aliyekunywa pombe aina ya gongo.Hata waliokuwepo wamelala nje walikuwa hawajitambui.Ole akaona huu ndio muda mzuri wa kukamilisha kazi yake kwa sababu watu wote walikuwa fofofo.

Endelea nayo…
Ole alijisogeza hadi kwenye Jeneza lililokuwa limeuhifadhi mwili wa mama Jesca.Alilifungua na kuitazama sura ya marehemu,kisha akalifunika Jeneza hilo.Aligeuza shigo yake na kuwatazama baba Jesca na watoto wake.Ole aliamua kutazama juu huku machozi yakimtoka.
Akajikuta anazungumza nafsini,,
"Nimeweka agano na Soyeti,lazima nifanikishe hili".
"Lakini mbona hawana hatia!!! ".
"Ila Soyeti ameniahidi mtonyo wa kutosha".
"Lakini nafsi inaniuma kuyafanya haya".
"Hakuna namna ngoja niifanye kazi nisepe fasta".
Basi baada ya kujiuliza hayo,aliamua kuushika mmoja kati ya Mishumaa iliyokuwa pembezoni mwa Jeneza.Kila mshumaa aliokuwepo pale ambao ulikuwa unawaka,ulikuwa umewekewa kisaani maalumu ili hata kama ikatokea umeisha usilete madhara yoyote ya moto.Baada ya kuwa ameushikilia mshumaa ule kwa kutumia mkono wake wa kushoto huku akiwa anatetemeka aliamua kuudondosha juu ya godoro na kisha kuondoka kwa haraka isiyo kifani.Moto ulianza kusambaa pole pole huku moshi mzito ukianza kusambaa chumbani humo.Tukio lile lilifanya baba Jesca na familia yake kushtuka kwa haraka baada ya moto kufika karibu na miili yao na kuanza kuwaunguza.Wote watatu walikimbilia mlangoni kwa lengo la kutoka nje ili kuyaokoa maisha yao.Katika hali isiyokuwa ya kawaida mlango ulionekana kufungwa wakati hapo awali ulikuwa wazi.Kumbe baada ya Ole kumaliza kufanya kazi yake aliamua kutoka na kuufunga mlango wa chumba hicho kwa nje.Kibaya zaidi moto ulizidi kusambaa kwa kasi ya ajabu huku moshi mzito ukizidi kurindima chumbani humo.
Walijikuta wanashindwa kupiga makelele kwa lengo la kuomba msaada kwa sababu ya wingi wa moshi.Kila mmoja alionekana kupumua kwa tabu hivyo ilikuwa ngumu kupaza sauti.Kwa sasa moto ulikuwa umesambaa chumba kizima.Baba Jesca na watoto wake walianza kupata mateso ya kushambuliwa na moto mwilini.Waliungua vibaya sana.Jeneza la marehemu lilionekana kuwaka moto kwa kasi sana.Ghafla kichwa cha marehemu kilipasuka na kutoa mlio mithili ya gurudumu la gari lililopata pancha.
ITAENDELEA USIKOSE.....

JIFUNZE KUPITIA HADITHI.

…JESCA……
Episode ya 3
Na:Esko Donald
Esko Wa Simulizi 'EWS'
Whatsapp:0675730796

Ilipoishia…
Mganga mfawidhi wa Zahanati hiyo aliamua iwe siri ili kulinda kibarua chake kisije kuota nyasi.Cha ajabu zaidi siku ambayo Soyeti alikuwa akifanya ubabazi kwa mama Jesca kumbe kulikuwapo nesi ambaye alibahatika kushuhudia tukio zima kupitia dirisha la nyuma la chumba hicho japokuwa Soyeti alijiridhisha kuwa hakukuwa na mtu mahali pale,alifeli.Nesi hiyo aliyefahamika kwa jina la Nasra hakuwa radhi kusema kwa kuhofia usalama wake.

Endelea nayo...
Hakuna mwanakijiji yoyote aliyefahamu haya.Wengi waliamini tatizo la kisukari ndilo lililopelekea umauti kwa mama Jesca.Inafahamika kuwa baada ya kifo kutokea mwili wa mama Jesca ulirejeshwa nyumbani kwa ajili ya taratibu za mazishi.Ulifikishwa nyumbani mnamo majira ya saa sita mchana.Vilio vya simanzi vilisikika kila kona,kila mtu alikuwa akisikitika ki vyake.Wengi waliumia kwa sababu marehemu aliishi vizuri na kila mtu kijijini hapo.
Taratibu za mazishi zilikamilika,kilichobaki alikuwa anasubiriwa Jesca afike ndio mazishi yafanyike.Usiku ulifika huku ndugu na jamaa wakiendelea kupeana faraja kwa kile kilichotokea kwamba ni kazi ya Mungu haina makosa.Muda wa kulala ulifika,ndipo mwili wa marehemu ukaingizwa ndani ya chumba ambacho ndicho walikuwepo baba Jesca na wadogo zake Jesca(Oropi na Songoi).Chini ya Sakafu kulionekana godoro aina Vita raha ambalo ndilo lilitumika kwa ajili ya kuwalaza baba Jesca na watoto wake.
Ilikuwa ni majira ya saa tisa usiku,kila mmoja alionekana kupitiwa na usingizi.
"Hakikisha unakamilisha kazi niliyokupa sawa".
"Nimekuelewa boss ondoa Shaka".
Haya yalikuwa ni mazungumzo kati ya Soyeti na kijana mmoja aliyefahamika kwa jina la Ole.Inaonekana kuna kazi ambayo Ole alitakiwa kuifanya usiku ule.
Kwa mwendo wa kunyatanyata,kijana Ole alikuwa anaelekea kwenye chumba ambacho walikuwepo baba Jesca na familia yake.Mlango wa chumba ulikuwa wazi hivyo ilikuwa ni raisi kwa mtu yoyote kuingia ndani.Ole alifanikiwa kuingia chumbani bila mtu yoyote kumuona.Bila shaka alikuwa anakwenda kukamilisha kazi aliyoambiwa aikamilishe.Kwa muda huo watu wote walikuwa wapo kwenye usingizi mzito unaweza kusema hawataamka tena,kila mmoja alikuwa anakoroma mithili ya mlevi aliyekunywa pombe aina ya gongo.Hata waliokuwepo wamelala nje walikuwa hawajitambui.Ole akaona huu ndio muda mzuri wa kukamilisha kazi yake kwa sababu watu wote walikuwa fofofo.
ITAENDELEA....... USIKOSE.
JE NI KAZI GANI OLE ALITUMWA KUIFANYA USIKU ULE?
MAJIBU YAPO KWENYE EPISODE YA 4.

JIFUNZE KUPITIA HADITHI.

……JESCA……
Episode ya 2
Na:Esko Donald.
Esko Wa Simulizi 'EWS'.
Whatsapp:0675730796.

Ilipoishia..
BAADA YA MIAKA MITATU.
Jesca anapokea simu na kuambiwa kifo cha wazazi wake pamoja na wadogo zake ni njama iliyofanywa na mtu wake wa karibu ambaye ni mpenzi wake,mvulana ambaye walipendana sana.Anaambiwa kuwa mpenzi wake ndiye amepelekea maafa haya kutokea.

Tuendelee Nayo.
Taarifa hizi zinakuwa mpya kwa Jesca na pia ilikuwa ngumu kuamini,ni kwa vipi mpenzi wake ndio chanzo cha haya yote,?,hilo lilikuwa swali lililokosa majibu fasaha.Jesca na mpenzi wake walitokea kijiji kimoja japo mpenzi wake familia yake ilikuwa na uwezo wa kifedha kijijini hapo kwa kumiliki mashamba baadhi.Inafahamika kilichomuuwa mama yake Jesca ni tatizo la kisukari na sio zaidi ya hapo,na pia inafahamika kuwa baba yake na wadogo zake Jesca walitekea kwa moto uliotokea bahati mbaya huku chanzo kikisemekana kuwa ni mshumaa uliodondokea juu ya godoro.
SIKU MBILI KABLA YA KIFO CHA MAMA JESCA.
Akiwa kwenye Zahanati ya kijiji,presha ya kupanda inaonekana kumuandama mama Jesca.Matatibu wanaonekana kutumia juhudi ya ziada kuipunguza presha hiyo kwa kumuwekea dripu za dawa.Baada ya muda kupita anakuja mpenzi wake na Jesca kwa lengo la kumjulia hali mama mkwe wake.Alifika na kumkuta akiwa amepitiwa na usingizi mzito.Mpenzi wake na Jesca alikuwa anaitwa Soyeti.Ndani ya chumba hicho hakukuwa na mtu mwengine zaidi ya Soyeti na Mama Jesca.Ghafla Soyeti alionekana kutupa macho huku na kule kutazama kama kuna mtu anakuja,baada ya kuona hali ni shwari,alizamisha mkono wake mfukoni na kutoa bomba la sindano ambalo ndani yake lilionekana kuwa na dawa.Aliamua kuichangana dawa hiyo kwa kuiingiza kwenye dripu ambalo lilikuwa na dawa ya kushusha presha.Ni wazi lengo la Soyeti lilikuwa ni kumuua mama Jesca kwani dawa aliyoitumia ilikuwa ni dawa ya kuogeshea ng'ombe kwa ajili ya kuua kupe inayofahamika kwa jina la Paranex.
Baada ya kufanikisha lengo lake,kwa haraka isiyo  mashaka anaamua kuondoka.Hali ya mama Jesca inabadilika ghafla na kupoteza maisha papo hapo.Baada ya kifo hicho kutokea uchunguzi ulifanyika na kufahamika kuwa mama Jesca aliuawa kwa sumu ila haikufahamika ni nani halihusika.Mganga mfawidhi wa Zahanati hiyo aliamua iwe siri ili kulinda kibarua chake kisije kuota nyasi.Cha ajabu zaidi siku ambayo Soyeti alikuwa akifanya ubabazi kwa mama Jesca kumbe kulikuwapo nesi ambaye alibahatika kushuhudia tukio zima kupitia dirisha la nyuma la chumba hicho japokuwa Soyeti alijiridhisha kuwa hakukuwa na mtu mahali pale,alifeli.Nesi hiyo aliyefahamika kwa jina la Nasra hakuwa radhi kusema kwa kuhofia usalama wake.
ITAENDELEA......... USIKOSE.

JIFUNZE KUPITIA HADITHI.

Na:Esko Donald.
Esko Wa Simulizi 'EWS'.

Jesca binti wa Kimasai mwenye rangi ya bahati kuliko mabinti wote kijijini kwao alikuwa ni mtoto wa kwanza kwenye familia ya watoto watatu yani yeye Jesca na wadogo zake wawili,Oropi na Singoi.
Uzuri wa Jesca haukujificha machoni pa wengi,kila mmoja alipenda kumtazama muda wote.Ilifika wakati vijana walikuwa wakisema kumtazama Jesca kwa dakika tano basi kutakuongezea maisha marefu duniani.Alama yake ya kidoti chenye rangi nyeusi usoni mwake kilinogesha uzuri wake.Maisha yalikuwa niya furaha sana kwenye familia yao.
Jesca anapata bahati ya kufika chuo kikuu kuchukua degree yake ya kwanza.Wazazi wa Jesca japokuwa walikuwa na maisha ya kawaida ila walijitahidi kumsomesha mtoto wao mpaka chuo kikuu.Alikuwa anachukua shahada ya udaktari wa wanyama.Akiwa Mwaka wa mwisho kuelekea kwenye mitihani ya kumaliza elimu yake anapigiwa simu na kupewa taarifa ya kifo cha mama yake mzazi.Jesca anajikuta anapoteza fahamu kwa masaa nane asijitambue.Baada ya muda kupita Jesca anarejewa na ufahamu asijue la kufanya kwa wakati huo.
Katika hali ya mshangao kunapigwa simu kutoka kijijini kwa kina Jesca na kutoa taarifa nyingine nzito ambayo iliupasua moyo wa Jesca na kulegeza viungo vyake vyote vya mwili wake.Ilikuwa ni taarifa nyingine ya msiba.Simu ilitoa taarifa juu ya kifo cha baba yake Jesca pamoja na wadogo zake wawili,kwa sasa familia nzima ya Jesca ilipoteza maisha.Baada ya kifo cha mama yake ambaye alikuwa anasumbuliwa na kisukari,maandalizi ya mazishi yalianza huku watu wakiwa wanamsubiri Jesca kwa ajili ya mazishi.Mwili wa mama yake Jesca baada ya kutoka hospitali moja kwa moja uliletwa nyumbani kwa ajili ya kutoa heshima za mwisho.Ilikuwa ni majira ya usiku mwili wa mama Jesca ukiwa ndani huku pembezoni mwake ukiwa umezungurushiwa mishumaa,ghafla mshumaa mmoja unadondoka chini ambapo ulikutana na godoro ambalo walikuwa wamelalia baba yake Jesca na wadogo zake.Kwa hali isiyokuwa ya kawaida nyumba nzima inawaka moto.Moto huo uliteketeza kila kitu ikiwemo mwili wa aliyekuwa marehemu mama Jesca,baba Jesca na wadogo zake.Hakuna kitu kilichotoka salama.Chumba ambacho familia ya Jesca ilikuwa imelala ndicho chumba ambacho mwili wa mama Jesca ulikuwa umehifadhiwa ndio maana ilikuwa rahisi wote kupoteza maisha.
Jesca alilia mpaka sauti ikapotea,alitamani iwe ndoto kwa haya yaliyomkuta.Aliyakumbuka maisha ya furaha aliyoishi na familia yake.Alitamani familia yake ile matunda kutoka kwake kwani walipambana kumsomesha.Kibaya zaidi kinachompa simanzi ni kukosa kuiona miili ya wazazi wake pamoja na wadogo zake kwa sababu iliteketea kwa moto na kubaki majivu.
BAADA YA MIAKA MITATU.
Jesca anapokea simu na kuambiwa kifo cha wazazi wake pamoja na wadogo zake ni njama iliyofanywa na mtu wake wa karibu ambaye ni mpenzi wake,mvulana ambaye walipendana sana.Anaambiwa kuwa mpenzi wake ndiye amepelekea maafa haya kutokea.
ITAENDELEA……….

Saturday, 23 September 2017

HATA WEWE ZINAKUHUSU:KINACHOMPATA EBITOKE MUDA HUU HAWEZI KUSAHAU.

Staa wa vichekesho,'Ebitoke',Kinachompata huko Instagram muda huu atakaa asahau.Hii imetokea baada ya kupost hii picha ya Hamisa na kuandika 'Happy Birthday Zari the boss Lady'.Mashabiki wa Zari wamemjia juu na kuanza kummiminia matusi ya kutosha.
Tembelea Instagram muda huu ujionee mwenyewe.
Na:Esko Donald.

Friday, 22 September 2017

HATA WEWE ZINAKUHUSU,JIONEE MAAJABU YA LEMMA GUYA GEMEDA.

Bila shaka ni wengi hatumfahamu Lemma Guya Gemeda,huyu ni mchoraji maarafu kutoka nchini Ethiopia.Lemma ana umri wa miaka 90 na amechora zaidi ya picha 10,000 ndani ya miaka zaidi ya sabini ambayo amekuwa akifanya kazi hii.Mzee huyu ni maarafu sana kutokana na picha zake ambazo huzichora kwenye ngozi zilizotoka kwa mbuzi au ng'ombe.
Hata picha hii ya mwanamke unayoiona amechora yeye.Kweli kipaji ni maarifa.
Na:Esko Donald.

HATA WEWE ZINAKUHUSU,TAZAMA MSIMAMO WA VIEWS YOU TUBE KATI YA ZILIPENDWA NA SEDUCE ME.

Leo nimekuletea msimamo wa views huko you tube kati ya hizi ngoma mbili yani Zilipendwa kutoka Wasafi na Seduce me kutoka kwa mkali Ali Kiba.
Na:Esko Donald.

JIFUNZE KUPITIA HADITHI.

…JESCA…… Episode 4 Na:Esko Donald Esko Wa Simulizi 'EWS' Whatsapp:0675730796 Ilipoishia… Kwa muda huo watu wote walikuwa wapo ...