Aliyekuwa Mfalme wa muziki wa Taarabu nchini Tanzania, Alhaj Mzee Yusuf jana usiku amefiwa na mke wake wa pili wa ndoa ajulikanae kwa jina la Chiku Khamis baada ya upasuaji (Operation) uzazi kutokwenda salama.
Mzee Yusuf amesema mke wake alianza kuugua uchungu wa uzazi kuanzia asubuhi jana na alipoona hali yake inazidi kuwa mbaya ndipo alipochukua uamuzi wa kumpeleka Hospitali ya Amana ambako alifanyiwa upasuaji na kwa bahati mbaya mtoto akazaliwa akiwa ameshafariki na muda mfupi baadae mama mzazi nae akaaga Dunia.
Source:Bongo5
Na:Esko Donald.
No comments:
Post a Comment