Msanii wa kizazi kipya 'Diamond Platinum' ameingia kwenye mining'ono ya vinywa vya Watanzania wengi kutokana na kuja na bidhaa yake ya perfume ijulikanayo kwa jina la "CHIBU PERFUME".Amesema ilimchukia takribani miaka miwili kufanikisha hili.Aliongeza na kusema kuwa bidhaa yake ina ubora wa hali ya juu ukilinganisha na perfume zingine.Bidhaa hiyo ambayo imetengenezwa nchini Dubai inauzwa Sh.105000.Kwa mujibu wa yeye mwenyewe alisema bei hii imezingatia na ubora wa bidhaa yenyewe.
Kwa sasa CHIBU PERFUME inafanya vizuri sokoni tofauti na mategemeo ya wengi.
Na:Esko Donald.
No comments:
Post a Comment