Rais wa Jamhuri ya Muungano Mh.John Pombe Magufuli ameipokea kwa mshtuko mkubwa taarifa ya vifo vya wanafunzi 32,wakiwemo walimu wawili na dereva.Ametuma salamu za rambi rambi kuonyesha kuguswa na hili.
Ajali hii ilitokea baada ya basi walilopanda wanafunza hawa kuacha njia na kuangukia kwenye Korongo,Karatu mkoani Arusha walipokuwa wanaenda kufanya mtihani wa ujirani mwema kwenye shule inayofahamika kwa jina la Tumaini.
Wanafunzi hawa wa darasa la saba waliopata ajali ni wanafunzi kutoka shule ya msingi ya Lucky Vicent.
Na:Esko Donald.
No comments:
Post a Comment